Jinsi ya Kupika Biriani ya Kuku Tamu
Jinsi ya Kupika Biriani ya Kuku Tamu
Jinsi ya Kupika Biriani ya Kuku Tamu
Viungo vya Mahitaji:
???? Kwa ajili ya kuku:
- 1 kg ya kuku, kata vipande
- 1 kikombe cha mtindi (yogurt)
- 2 nyanya kubwa, blend
- 1 kitunguu maji kikubwa, kata vipande vidogo
- 1 kijiko cha chai cha tangawizi ya kusagwa
- 1 kijiko cha chai cha kitunguu saumu cha kusagwa
- 1 kijiko cha chai cha garam masala
- 1 kijiko cha chai cha manjano (turmeric)
- 1 kijiko cha chai cha pilipili mbuzi (hiari)
- Chumvi kiasi
- Mafuta ya kupikia
???? Kwa ajili ya wali:
- 3 vikombe vya mchele wa Basmati
- 5 vikombe vya maji
- 1 kijiko cha chai cha bizari ya pilau
- 2 karafuu
- 2 iliki
- 1 kijiti cha mdalasini
- Chumvi kiasi
- Mafuta ya samli (ghee)
???? Kwa ajili ya mapambo:
- Viazi vya kukaanga
- Mayai ya kuchemsha
- Kotmiri (coriander) iliyokatwa
Maelekezo:
Hatua ya 1: Kupika Kuku
- Katika bakuli, changanya kuku na mtindi, tangawizi, kitunguu saumu, garam masala, manjano, pilipili mbuzi na chumvi. Acha iroweke kwa dakika 30.
- Kaanga vitunguu mpaka viwe na rangi ya kahawia kisha weka nyanya ya ku-blend.
- Ongeza kuku ulio-marinate na pika hadi viungo viive vizuri na supu ipungue.
Hatua ya 2: Kupika Wali
- Osha mchele wa Basmati kisha uroweke kwa dakika 20.
- Chemsha maji kisha ongeza bizari, mdalasini, iliki, karafuu na chumvi.
- Weka mchele na pika mpaka uwe umeiva lakini sio kupitiliza. Chuja maji yote.
Hatua ya 3: Kuchanganya Biriani
- Katika sufuria safi, weka tabaka la wali, kisha tabaka la kuku, rudia hadi umalize.
- Funika na upike kwa moto mdogo kwa dakika 10-15 ili biriani ichanganyike vizuri.
Hatua ya 4: Kupamba na Kutumikia
- Mwagia mafuta ya samli juu, pamba kwa viazi vya kukaanga, mayai na kotmiri.
- Tumikia na kachumbari au raita.
???? Siri ya biriani tamu ni kupika mchuzi mzito wenye viungo vya kutosha na kuhakikisha mchele hauivuki. ????????